top of page

SEMINA

Masomo Bunifu ya Biblia

yanatumika vizuri kupitia semina na warsha

 

Walimu wa watoto na watoto wenyewe watafaidika sana ikiwa Masomo Bunifu ya Biblia yataeleweka na kutambuliwa. Tunaendesha semina na warsha ili kuwawezesha walimu kupata uwezo huu. Semina zinaweza kupangwa kwa muda wa siku mbili hadi nne, zipo za aina mbili tofauti.

Kozi ya msingi:

- Kanuni za Kibiblia za kuwafundisha watoto

- Kuwajua watoto tunaowafundisha (Saikolojia ya watoto)

- Mbinu za ufundishaji

- „Demo-lessons“ – wanasemina wanamtazama mwalimu anavyowafundisha             watoto na watafundisha wenyewe wakitumia Masomo Bunifu ya Biblia

- Watajifunza namna ya kutengeneza zana za kufundishia

Warsha ya wawezeshaji wa walimu wa Masomo Bunifu ya Biblia (ToT)

- Mungu, Yesu na Roho Mtakatifu kama walimu

- Mbinu za na namna ya kutambulisha muhtasari ya MBB na kuwafundisha walimu   wengine.

- Mazoezi darasani

- Baada ya ToT wawezeshaji watafundisha kozi ya msingi ya MBB wakiongozwa na   wawezeshaji wao.

 

Namna ya kupata semina?

- Tuma e-mail na eleza mahitaji ya kanisa / shirika lako, wahusika watakutumia         maelezo zaidi.

- Angalia kwenye orodha ya semina zilizopangwa tayari na wasiliana nasi. Labda       kuna nafasi kujiunga pale.

bottom of page